Mzigo-TV-728x90

Masomo ya misa

Masomo ya Misa Feb 20

By

on

Tumsifu Yesu Kristu… Karibu Katika Masomo ya Misa Takatifu 20/02/2024

2024 FEBRUARI 20 JUMANNE: JUMA LA 1 LA KWARESIMA
Mwenyeheri Yasinta
Urujuani
Zaburi: Juma 1

Somo 1. Isa 55: 10-11

Bwana asema: Kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.

Wimbo wa Katikati. Zab 34:4-6, 16-19

1. Mtukuzeni Bwana pamoja nami,
Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Nalimtafuta Bwana akanijibu,
Akaniponya na hofu zangu zote. (K)

(K) Wenye haki, Bwana anawaponya
        na taabu zao zote.

2. Wakamwelekea macho wakatiwa nuru,
Wala nyuso zao hazitaona haya.
Maskini huyu aliita, Bwana akasikia,
Akamwokoa na taabu zake zote. (K)

3. Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki,
Na masikio yake hukielekea kilio chao.
Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya,
Aliondoa kumbukumbu lao duniani. (K)

4. Walilia, naye Bwana akasikia,
Akawaponya na taabu zao zote.
Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,
Na waliopondeka roho huwaokoa. (K)

Injili. Mt 6: 7-15

Siku ile Yesu aliwaambia wafuasi wake: Mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu maneno yao kuwa mengi. Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnavyohitaji kabla ninyi hamjamwomba. Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. Utupe leo riziki yetu. Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

TAFAKARI

TUTULIE KATIKA SALA NA BWANA ATATUTIMIZIA HAJA ZETU: Katika maisha yetu, tuna mahitaji mbalimbali ambayo tunahitaji kutoka kwa Mungu. Ni kwa njia ya sala iliyo bora na yenye utulivu, Mungu anatutimizia mahitaji yetu. Injili Takatifu inatupa mfano wa utulivu katika kusali kwa njia ya maonyo kwa wafuasi wa Yesu, kwamba wasiwe kama watu wa mataifa. Wanaambiwa wasipayuke payuke, yaani namna hii inawataka wawe na utulivu. Pia Yesu aliwapa mfano wa namna ya kusali, ndio sala ya Baba yetu. Utulivu huu katika sala hupelekea kujibiwa shida zetu kwani maombi yetu humfikia Mungu na wala hayarudi. Namna hii inashuhudiwa na nabii Isaya ya kuwa Neno la Mungu litatimia wala halitarudi na litatimiliza haja zetu. Wapendwa, katika sala tuliyoishuhudia ina namna mbalimbali za kuzungumza na Mungu kwa utulivu, inamsifu na kumtukuza Mungu, inatoa shukrani kwa Mungu, inaeleza maombi ya mahitaji, na kudhihirisha namna ya kusameheana. Nasi tujifunze katika hayo ili pindi tusalipo tusali kwa utulivu hali tukiweka wazi malengo yetu ya sala.

SALA: Ee Bwana Yesu, tunakuomba utufundishe kusali jinsi vile itupasavyo. Amina. 

About mzigotv

Nyimbo Mpya 2023, 2022 Download Audio, Video, Mp3, Mp3 African music, Tanzania Music, Naijamusic, naijavibe, Bekaboy, Djmwanga, Tanzania songs, Kenya songs, Uganda songs, Rwanda songs, Congo songs, Zanzibar, Singeli, Taarabu, Reggae, Amapiano, Nyimbo za dini, Gospel songs, Diamond platnumz, jux, Rayvanny, Harmonize, Nandy, Zuchu, Wasafi, Alikiba Teading songs, Top 100 songs youtube, Nigeria, Naija songs.

Recommended for you