Mzigo-TV-728x90

Masomo ya misa

Masomo ya Misa Oktoba 4

By

on

Tumsifu Yesu Kristo. Karibu Katika Masomo ya Misa 04/10/2024

2024 OKTOBA 4: IJUMAA-JUMA LA 26 LA MWAKA

Fransisko wa Asizi
Rangi: Nyeupe

Zaburi: Juma II

SOMO 1. Ayu 38:1, 12-21, 40:3-5

Ndipo Bwana alimjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema, Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza? Umeyajulisha mapambazuko mahali pake? Yapate kuishika miisho ya nchi, waovu wakung’utwe wakawe mbali nayo? Hubadilika mfano wa udongo chini ya muhuri, vitu vyote vinatokea kama mavazi. Na waovu nuru yao huzuiliwa isiwafikie, na mkono ulioinuka huvunjika. Je! Umeziingia chemchemi za bahari, au umetembea mahali pa siri pa vilindi? Je! Umefunuliwa malango ya mauti, au umeyaona malango ya kuzimu? Umeyafahamu mapana ya dunia? Haya! Sema, ikiwa unayajua hayo yote. “Iko wapi njia ya kuyafikia makao ya nuru? Na giza pia, mahali pake ni wapi? Upate kuipeleka hata mpaka wake, upate kuelewa na mapito ya kuiendea nyumba yake? Hukosi unajua, maana ulizaliwa wakati huo, na hesabu ya siku zako ni kubwa! Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema, Tazama, mimi si kitu kabisa, nikujibu nini? Naweka mkono wangu kinywani pangu. Nimenena mara moja, nami sitajibu; naam, nimenena mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”

WIMBO WA KATIKATI. Zab 139:1-3, 7-10, 13-14

1. Ee Bwana umenichunguza na kunijua.
Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;
Umelifahamu wazo langu tokea mbali.
Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu,
Umeelewa na njia zangu zote.

(K) Uniongoze Bwana, katika njia ya milele.

2. Niende wapi nijiepushe na roho yako?
Niende wapi niukimbie uso wako?
Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko;
Ningefanya kuzimu kitanda change, Wewe uko. (K)

3. Ningezitwaa mbawa za asubuhi,
Na kukaa pande za mwisho za bahari;
Huko nako mkono wako utaniongoza,
Na mkono wako wa kuume utanishika. (K)

4. Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu,
Uliniumba tumboni mwa mama yangu.
Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa
Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. (K)

INJILI. Lk 10: 13-16

Yesu aliwaambia wafuasi wake: “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza hiyo iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu tangu hapo, huku wakiketi katika nguo za kigunia na majivu. Lakini, siku ya hukumu itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zake kuliko ninyi. Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa hata mbinguni? Utashushwa hata kuzimu. Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”

TAFAKARI

WITO WA KUSIKILIZA: Ikiwa heshima huwaendea madaktari na wakufunzi. Ikiwa utajiri, mali na mafanikio huwaendea wakurugenzi na wanasheria, ikiwa umaarufu huwaendea wanamichezo, wanamuziki, waigizaji wanaogonga vichwa vya habari, je! Waandishi wa Injili wanapata kitu gani? Wao wanapata ujumbe ambao unawapatia uzima wa milele. Lakini kama wainjili hao watakataa kuupeleka ujumbe huo wa Habari njema kwa wengine watatengwa milele na Mungu. Ikiwa kuna kazi ya muhimu ambayo inatakikana kufanyika kwa njia au kwa gharama yoyote ile, basi inapaswa ifanywe kwa namna tofauti, kwa weledi na kipekee kabisa. Fursa na wajibu wetu sisi tulio wafuasi wake ni kutangaza Habari njema. “Yesu aliwaambia wafuasi wake: “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza hiyo iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu tangu hapo, huku wakiketi katika nguo za kigunia na majivu.” Na kwa maneno ya Paulo mtume; “Ole wangu kama nisipohubiri Injili.”

SALA: Bwana Yesu utujalie fadhila ya kuwasikiliza unaowatuma kwenu.

About mzigotv

Nyimbo Mpya 2025 2024 2023 2022 Download Audio, Video, Mp3, Mp3 African music, Tanzania Music, Naijamusic, naijavibe, Bekaboy, Djmwanga, Tanzania songs, Kenya songs, Uganda songs, Rwanda songs, Congo songs, Zanzibar, Singeli, Taarabu, Reggae, Amapiano, Nyimbo za dini, Gospel songs, Diamond platnumz, jux, Rayvanny, Harmonize, Nandy, Zuchu, Wasafi, Alikiba Teading songs, Top 100 songs youtube, Nigeria, Naija songs.

Recommended for you