Mzigo-TV-728x90

Masomo ya misa

Masomo ya Misa Machi 9

By

on

Tumsifu Yesu Kristu… Karibu Katika Masomo ya Misa 09/03/2024

2024 MACHI 9 JUMAMOSI: JUMA 3 LA KWARESIMA
Mt. Fransiska wa Roma 
Urujuani
Zaburi: Juma 3

Somo 1. Hos 6:1-6

Bwana asema: ”Katika taabu yao watanitafuta kwa bidii: Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.” Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake. Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi. Ee Efrahimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema. Kwa sababu hiyo, nimewakata-kata kwa vinywa vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa changu; na hukumu yangu itatokea kama mwanga. Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.

Wimbo wa Katikati. Zab 51:3-4, 18-21

1. Ee Mungu, unirehemu,
Sawasawa na fadhili zako.
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
Unioshe kabisa na uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu. (K)

(K) Ninavyotaka ni fadhili, si sadaka.

2. Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,
Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;
Moyo uliovunjika na kupondeka,
Ee Mungu, hutaudharau. (K)

3. Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,
Uzijenge kuta za Yerusalemu.
Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,
Na sadaka za kuteketezwa, na kafara (K)

Injili. Lk 18:9-14

Yesu aliwaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. ”Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; ”Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang`anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato  yangu yote.” Lakini yule mtoza ushuru alisisima mbali, wala hakudhubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, ”Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.” Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhilie atakwezwa. 

TAFAKARI

DHARAU MWISHO WAKE MAJUTO: Kama kuna sala inayofika kwa Mungu kwa haraka ni ‘sikitiko la mnyonge sababu ya kuonewa, kudhalilishwa na kukosa haki.’ Mwanadamu akifanikiwa wakati mwingine hujisahau na kuanza kudharau na kudhalilisha wengine. Huo tunaweza kuuita ni Ufarisayo. Huyu Mfarisayo alijiona kuwa bora kuliko yule mtoza ushuru na kuanza kujisifia kwa litania ya majigambo, oh mimi niko 1,2,3, mimi nina 1,2,3 na mbaya zaidi kusema, ‘mimi sio kama akina fulani wala kama huyu mtoza ushuru’. Mara nyingi wasio nacho hugandamizwa na walio nacho kiuchumi/kimadaraka. Kuna baadhi wakijaliwa hawaambiliki, wanajikweza na kujiona mungu mtu, wanajisahau na kudhani ni kwa nguvu zao, au wanastahili kuliko wengine, Mungu anakosa nafasi katika maisha yao, wanakosa unyenyekevu, wanajiona kuwa wao ni binadamu zaidi ya wengine. Tumwangalie huyu Mfarisayo na tujifunze kitu. Je, kwa kujua la mwenzako ndio unalitangaza? Tuko ambao tunaposali tunawaangalia wengine kwanza wanafanyaje. Huo ni ulemavu wa kiroho.

SALA: Ee Baba wa huruma, utuhurumie sisi wakosefu.

About mzigotv

Nyimbo Mpya 2023, 2022 Download Audio, Video, Mp3, Mp3 African music, Tanzania Music, Naijamusic, naijavibe, Bekaboy, Djmwanga, Tanzania songs, Kenya songs, Uganda songs, Rwanda songs, Congo songs, Zanzibar, Singeli, Taarabu, Reggae, Amapiano, Nyimbo za dini, Gospel songs, Diamond platnumz, jux, Rayvanny, Harmonize, Nandy, Zuchu, Wasafi, Alikiba Teading songs, Top 100 songs youtube, Nigeria, Naija songs.

Recommended for you