Tumsifu Yesu Kristo. Karibu Katika Masomo ya Misa 27/10/2024
2024 OKTOBA 27: DOMINIKA YA 30 YA MWAKA
Rangi: Kijani
Zaburi: Juma II
SOMO 1. Yer 31: 7-9
Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako mabaki ya Israel. Tazama, nitawaleta toka nchi ya kaskazini, na kuwakusanya katika miisho ya dunia, na pamoja nao watakuja walio vipofu, na hao wachechemeao, mwanamke mwenye mimba, na yeye pia aliye na utungu wa kuzaa; watarudi huko, jeshi kubwa. Watakuja kwa kulia, na kwa maombi nitawaongoza; nitawaendesha penye mito ya maji, katika njia iliyonyoka; katika njia hiyo hawatajikwaa; maana mimi ni baba wa Israeli, na Efraimu ni mzaliwa wa kwanza wangu. |
WIMBO WA KATIKATI. Zab 126
1. Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, (K) Bwana alitutendea mambo makuu, tulikuwa tukifurahi. 2. Ndipo mataifa waliposema, 3. Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa, |
SOMO 2. Ebr 5: 1-6
Ndugu, kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi; awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu, na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi. Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni. Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. Kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki. |
INJILI. Mk 10: 46-52
Yesu alipokuwa akishika njia kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano mkubwa, mwana wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa ameketi kando ya njia. Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu. Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, mwana wa Daudi, unirehemu. Yesu akasimama akasema, mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita. Akatupa vazi lake, akaruka, akamwendea Yesu. Yesu akamjibu, akamwambia, Wataka nikufanyie nini? Yule kipofu akamwambia, Mwalimu wangu, nataka nipate kuona. Yesu akamwambia, Enenda zako, imani yako imekuponya. Mara akapata kuona; akamfuata njiani. |
TAFAKARI
KRISTO KUHANI MKUU: KWA NJIA YAKE TUMEUHISHWA UPYA SALA: Ee Bwana Yesu utufanye tuweze kuona kiimani ili tuyatukuze matendo yako makuu. |
The post Masomo ya Misa Dominika ya 30 appeared first on CLARETIAN PUBLICATIONS-EAST AFRICA.