Habari

Simba SC, Azam FC, Young Africa zakwepana ASFC

By

on

 

Mabingwa Watetezi wa Kombe la Shirikishso Tanzania Bara ‘ASFC’ Young Africans wamepangwa kucheza dhidi ya Geita Gold FC katika mchezo wa Robo Fainali ya Michuano hiyo msimu huu 2022/23.

Young Africans ambayo ilitwaa ubingwa wa michauno hiyo msimu uliopita kwa kuifunga Coastal Union kwa changamoto ya mikwaju ya Penati baada ya sare ya 3-3 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid-Arusha, itacheza mchezo huo wa Robo Fainali nyumbani jijini Dar es salaam.

Geita Gold FC watakuwa na kazi kubwa ya kulipa kisasi dhidi ya Wananchi, hasa ikizingatiwa mwishoni mwa juma lililopita ilikubali kichapo cha 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Uwanja wa Azam Complex Chamazi.

Harry Kane kuzichonganisha Spurs, Man Utd

Mbali na mchezo huo wa Ligi Kuu, Geita Gold FC itakuwa inakumbuka mchezo wa Robo Fainali wa ‘ASFC’ dhidi ya Young Africans uliopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam msimu uliopita 2021/22. Mchezo huo ulishuhudia Geita Gold FC ikipoteza kwa changamoto ya mikwaju ya Penati.

Meneja Arsenal amtahadharisha Gabriel Jesus

Michezo mingine ya Robo Fainali ya ASFC iliyopangwa leo Jumatano (Machi 15) kupitia Droo iliyofanyika Studio za Azam Media jijini Dar es salaam.

Simba SC 🆚 Ihefu SC

Singida Big Stars 🆚 Mbeya City

Azam FC 🆚 Mtibwa Sugar

About mzigotv

Nyimbo Mpya 2022, Mp3 Mp4 Mzigotv, Audio, Video Mpya, Tanzania Mp3, Tanzania trending songs, Nyimbo Mpya 2022, 2021, Download Audio Mzigotv, Alikiba Mp3, Video, Dj mwanga, nyimbo mpya za wiki hii dj mwanga, Rayvanny, Harmonize, Diamond Platnumz, Alikiba, Jux, Nandy, Zuchu, Lavalava, Mbosso, Bekaboy, Yingamedia, Diamond Platnumz Songs 2022


Notice: Trying to get property of non-object in /home/tjsxvbmy/public_html/wp-content/themes/osage/functions.php on line 1056

Notice: Trying to get property of non-object in /home/tjsxvbmy/public_html/wp-content/themes/osage/functions.php on line 1060

Recommended for you